Sunday, May 1, 2011

Yohana Apata WheelChair Nyingine Toka Canada




 Aliahidiwa wiki jana na Raia Mwema aliye Canada. Atakuja nayo Juni 3. Nimewasiliana na mlezi wa Yohanna Bw. Revocatus na tumekubaliana, kuwa , katika kipindi hiki mpaka Juni 3, kama Yohanna atapewa wheel chair nyingine, basi, itakayokuja apewe muhitaji mwingine. Maana, wenye kuhitaji wheelchair ni wengi.
Chini hapa ni ujumbe kutoka kwa Raia Mwema huyu aliye Canada;

Kaka Mjengwa, 

Nilifanikiwa kupata ile baiskeli napicha ni hizo hapo juu huyo ni
jamaa aliyeniuzia.

Kama nilivyosema mwanzo ni baiskeli ambayo imetumika lakini nimeridhika sana
hali yake.

Nashukuru kwa wadau wengine walioweza kujitolea msaada wa baiskeli kwa kaka
Yohana.

Tuwasiliane zaidi.


Asante.