Saturday, April 23, 2011

Mama Na Mtoto Wafa Katika Ajali Ya Basi Morogoro

Basi la Kampuni ya Mabsi ya Al-Saedy likiwa limepinduka  Sanga Sanga mkoani morogoro jana jioni

Majeruhi akihudumiwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro
 Abiria walionusurika katika ajali hiyo                                                                                     MAMA na mtoto wamefariki dunia papo hapo huku abiria 30 wakijeruhiwa baada ya basi waliokuwa wakisafiria la kampuni ya Al-Saedy lililokuwa likitoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam kupata ajali iliyohushwa na lori na kupinduka eneo la Sangasanga kwa Mwarabu katika wilaya ya Mvomero barabara kuu ya Iringa-Morogoro mkoani hapa.                                                                                                                                                     Ajali hiyo  ilitokea Majira ya 11:45 jana jioni katika eneo hilo Ambapo basi lenye namba ya usajili T 267 AWG Scania mali ya kampuni ya Al-Saedy yenye makao makuu mkoani Morogoro ilikuwa linaendeshwa na dereva Erick Luoga ikitokea mkoani Mbeya kuelekea Dar es Salaam iligongana na lori lenye namba ya usajili T 346 ABX Scania likiwa na tela T 657 AGU mali ya kampuni ya Trans Cargo ya Dar es Salaam lililokuwa likiendeshwa na dreva, Ally Khamis (48) mkazi wa Kigogo Jijini Dar es Salaam ilisababisha vifo vya abiria wawili ambao ni mama na mtoto wake.(Habari na Picha: Juma Mtanda)